www.nipetanosolowa.blospot.com

Wednesday, August 22, 2012

MATIKIO YA IDD EL FITRI NDANI YA UKUMBI WA DAR LIVE........................

                          Wasanii wa Bongo flavour,kutoka kushoto Linah,Mwansiti na Maunda Zorro.
                              Maunda Zorro akiwa katika stage ndani ya ukumbi wa Dar Live.
                    Msanii Mwansiti akipiga shoo ndani ya Dar Live.

Monday, August 20, 2012

MSANII DARASA ANAMALIZIA MOVIE YAKE YA WIMBO WAKE "SIKATI TAMAA"

           Msanii wa bongo flavour akiwa katika pozi,anafanya movie ya wimbo wake "sikati tamaa"
      hiyo ni sehemu ya shot ya movie hiyo ya sikati tamaa.
        Msanii Godzilla a k a King zilla akiwa katika shot ya movie ya sikati tamaa,Wasanii kibao na watu maarufu watakuwepo katika movie hiyo ya sikati tamaa.
    

PATA MATOKEO YA MECHI ZA LIGI UINGEREZA NA HISPANIA......

Wigan 0-2 Chelsia,Man City 3-3 Southampon(Uingereza)Real Madrid 1-1 Valencia,Atlentico Bilbao 3-5 Real Betis,Barcelona 5-1 Real Sociedad(Hispania).







LOVENESS LOVE DIVA AFUNGUKA.........

Mcheki diva afunguka live.

WAISLAMU WANASHEREHEKEA SIKUKUU YA IDD EL FITR NA PIA BLOG YAKO YA NIPETANOSOLOWA TUNAWATAKIA WAISLAM WOTE DUNIANI IDD MUBBARAKA.

      Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Yusuph Mwenda wakati akiwasili kwenye msikiti wa Kinondoni kusali swala ya idd el Fitr.
      Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya mashekh kabla ya swala ya idd el fitr.
      Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mkono wa idd el fitr na waumini wenzake wa kiislam baada ya swala ya idd el fitr katika msikiti wa Kinondoni,jijini Dar es salaam.

Thursday, August 16, 2012

FABRICE MWANBA ASTAAFU SOKA...........

   Mchezaji wa Bolton Fabrice Muamba aliyeanguka uwanjani baada ya moyo wake kusimama kufanya kazi kwa muda wa masaa 72 kwenye mechi ya march 2012 ametangaza kustaafu soka miezi mitano baada ya kutokea tukio hilo.Fabrice Muamba  mwenye umri wa miaka 24 ameiambia tovuti ya club yake kwamba bado anazidi kushukuru mungu kwamba bado yupo hai na pia amewashukuru madaktari waliomsaidia.



WAWAKILISHI WETU TANZANIA KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI WAMEREJEA............

          Wawakilishi wa mchezo wa kuogelea Amal Gadiale(mbele) na Magdalena Moshi wakiwasili uwanja wa ndege jijini Dar es salaam.
      Rais wa kamati ya olimpiki Bw. filbert bayi akibadilishana mawazo na mkurugenzi wa michezo nchini Leonard Tadeo ambae alifika kuwapokea wawakilishi wa michezo ya olimpiki uwanja wa ndege jijini Dar es salaam.

Sunday, August 12, 2012

DOKTA ULIMBOKA AREJEA NCHINI,AMESEMA YUPO FIT.

Picha chini:Kiongozi wa jumuiya ya Madaktari nchini Tanzania Dkt Steven Ulimboka akiwa amebeba maua  na kuzungukwa na madaktari wenzake na wananchi wa kawaida waliofika kumlaki mara baada ya kuwasili mapema leo Augost 12,2012 kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea kwenye matibabu nchini Afrika ya Kusini.Dkt Ulimboka alisema kuwa kwa sasa yupo fit na anaweza kufanya shughuli zozote.   

GARI ANALOMILIKI MBWANA SAMATA.

      Mbwana samata akiwa katika gari.
                          Mchezaji wa TP Mazembe Mbwana samata.
           Mbwana samata akiwajibika katika moja ya mechi ya kimataifa ikiwa na timu yake ya taifa Tanzania.


   Mchezaji Mbwana Samata aliuzwa kwa dola za kimarekani zaidi ya 100,000 kwenda TP Mazembe kutoka timu ya Simba SC ya Tanzania.Mbwana Samata kwa sasa analipwa dola 5000 kwa mwezi ambayo ni sawa na Tsh Mil 7.5.

  Kwasasa amenunua gari la kisasa zaidi chrysler crossfire la mwaka 2006 ambalo limemgharimu takriban milion 50 za Kitanzania.Mbwana samata anaendelea kuonesha uwezo wa juu katika timu yake ya TP Mazembe.

VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AUG 12.























Saturday, August 11, 2012

KAZI FEKI ZA WASANII WA BONGO ZAKAMATWA.

Mkurugenzi wa kampuni ya msama promotion Mr Alex Msama naendeleza harakati za kuhakikisha wasanii wa Tanzania angalau wanafaidika na kazi zao baada ya kufanikisha kukamatwa kwa kopi feki za kazi za wasanii wa hapa nchini,Hapa Tanzania wasanii hawanufaiki na kazi zao,hii ni kutokana na wizi uliokithiri wa kazi zao,harakati alizo kuwa nazo Mr Msama kwa kushirikiana na jeshi la polisi inaonekana kupunguza makali ya wizi wa kazi za wasanii hapa nchini huku wakiwa wanasubiri kupitishwa kwa sheria ya hati miliki ambayo ndio kilio cha wasanii hapa nchini,Pia mdau wa sanaa hapa nchini unashauriwa kuto nunua kazi ambayo ni feki kwani hufanya wasanii wetu kuto nufaika na kufanya kupunguza kasi ya maendeleo.Kwakweli inasikitisha sana kuona msanii anaandaa kazi kwa mamilioni ya pesa kisha unakuta kazi feki inayouzwa tena mpaka shilingi elfu moja,huu ni unyonyaji mkubwa ambao tunatakiwa kuupinga vikali kwa kununua nakala ya kazi ya msanii original.